BIASHARA YA USAFIRISHAJI MAJINI
MAELEZO MAFUPI YA KAZI ZA DSB - KISWAHILI
1.0 KURUGENZI YA BIASHARA YA HUDUMA ZA MELI
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kupitia kurugenzi ya Biashara ya huduma za meli inatekeleza jukumu la Uwakala wa forodha chini ya sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania kifungu namba 7 Sura 415.
2.0 MAWANDA YA UWAKALA WA FORODHA
TASAC imepewa jukumu la kipekee la uwakala wa forodha kugomboa na kuondosha shehena zinazoingizwa au kutoka nchini kwa bidhaa zifuatazo:
- Silaha na vilipuzi;
- Makinikia;
- Kemikali zinazotumika kwenye kampuni za uchimbaji madini;
- Nyara za Serikali; na
- Wanyamapori kama walivyoainishwa kwenye Sheria ya Uhifadhi wa Wanyama Pori.
- KAZI ZA UWAKALA WA FORODHA
Kazi za uwakala wa forodha chini ya TASAC zinahusisha:
- kuhakiki nyaraka za uingizaji na uondoshaji shehena
- kuratibu ufuatiliaji wa vibali kutoka mamlaka mbalimbali
- kuandaa kadhia kupitia mifumo ya forodha
- kufuatilia malipo ya kodi
- kufuatilia nyaraka za usafiri na usafirishaji kutoka kwa wakala wa meli
- Kushiriki ukaguzi wa shehena kwenye maeneo ya kiforodha
- kuratibu na kufuatilia ankara za malipo ya gharama za bandari.
- Kuratibu usafirishaji wa shehena
- Kutoa ushauri kwa waagizaji na wasafirishaji wa shehena kuhusu taratibu za kiforodha kwa shehena zinazoingia au kutoka nchini.
MAENEO YA UWAKALA WA FORODHA
Huduma za uwakala wa forodha zinafanyika katika maeneo yafuatayo:
- Bandari
- Viwanja vya ndege
- Mipakani na,
Maeneo mengine yaliyoidhinishwa na Idara ya Forodha
MAWASILIANO
Unaweza kuwasiliana nasi kupitia anuani na namba za simu zifuatazo;
- Baruapepe;
- uingizaji wa shehena: importcfa@tasac.go.tz
- uondoshaji wa shehena: exportcfa@tasac.go.tz.
- vibali: group.cfatbs@tasac.go.tz
- huduma za wakala wa meli group.cfashipping@tasac.go.tz
- taarifa: info@tasac.go.tz
- Namba za simu
+255 222 127 313
+255 222 127 314
+255 222 340 006
+255 737 792 444