TASAC yashiriki Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma
TASAC yashiriki Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma
Imewekwa: 18 June, 2024
![TASAC yashiriki Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma](https://www.tasac.go.tz/uploads/news/6ea2a1261665d8273660aab311ad4e0e.jpeg)
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) ni moja ya Taasisi zinazoshiriki katika Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Viwanja vya Chinangali Park, Jijini Dodoma.
Maonesho hayo yameandaliwa kwa lengo la kukutanisha taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi, vyama vya ushirika na wadau kwa ujumla ili kuweza kutoa elimu juu ya shughuli mbalimbali wanazozifanya.
Maonesho hayo yameanza tarehe 16 Juni, 2024 na yanatarajia kuhitimishwa tarehe 23 Juni, 2024.