Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania

ISO 9001:2015 Certified

KATIBU TAWALA MKOA WA GEITA AIPONGEZA TASAC

Imewekwa: 01 October, 2025
KATIBU TAWALA MKOA WA GEITA AIPONGEZA TASAC

Katibu Tawala mkoa wa Geita  Mohamed Gombati amepongeza Shirika la Uwakala wa Meli  Tanzania (TASAC) kwa utoaji huduma bora ya udhibiti wa vyombo vya usafiri  majini na uvuvi mkoani humo.

Ameyasema hayo tarehe 26 Septemba, 2025 wakati alipotembelea banda la  TASAC katika maonyesho ya 8 ya teknolojia ya madini yaliyoanza tarehe 18  na kilele chake ni tarehe  28 Septemba, 2025 hapa Geita.

"Hongereni TASAC kwa kazi mnayofanya ya ukaguzi na udhibiti katika usafiri majini. Nashukuru  sana jinsi mlivyoshughuli changamoto za kisiwa cha Izmacheli maeneo ya  Nkome. Ushirikiano ni mzuri na unawafanya wananchi  wawe na imani na  ninyi". Amesema Gombati
 
Pia, Gombati ameahidi Serikali ya mkoa itaendelea kutoa ushirikiano na msaada wa karibu utakaohitajika kwa ajili ya kutatua changamoto ya matumizi ya vifaa okozi na kuhakikisha usafiri majini unaendelea kuwa salama ili kuwawezesha wananchi katika shuguli zao za kujipatia maendeleo.

Mrejesho, Malalamiko au Wazo