Naibu Waziri Uchukuzi kutembelea banda la TASAC
Naibu Waziri Uchukuzi kutembelea banda la TASAC
Imewekwa: 16 January, 2024
Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Mwakiposa Kihenzile ametembelea banda la Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) leo tarehe 8 Disemba, 2023 katika kilele cha Mkutano na maonesho ya 16 ya wadau wa Sekta ya Uchukuzi yanayofanyika Mkoani Arusha yaliyoanza tarehe 5-8 Disemba, 2023 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa jijini Arusha (AICC).
Mhe. Kihenzileya amepata maelezo kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Umma Mwandamizi, Bi. Amina Miruko kuhusu kazi zinazofanywa na Shirika hilo na kuiopongeza TASAC kwa huduma bora na salama za udhibiti katika sekta ya usafiri na usafirshaji kwa njia ya maji.